Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Maelfu wapata chanjo ya corona Dar, siku zaongezwa
Habari Mchanganyiko

Maelfu wapata chanjo ya corona Dar, siku zaongezwa

Spread the love

ZAIDI ya wananchi 2,882 mkoani Dar es Salaam, leo Jumapili tarehe 22 Agosti 2021, wamepata chanjo ya ugonjwa wa corona (UVIKO-19), katika Uwanja wa Uhuru, mkoani humo.Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla, wakati zoezi hilo likiendelea uwanjani hapo.

“Hadi saa 4.00 asubuhi tayari wananchi 2,882 walikuwa wamepokea chanjo. Kila aliyepokea chanjo amepatiwa cheti kinachotambulika kimataifa,” amesema Makalla.

Kufuatia mwitikio huo mkubwa wa wananchi kupata chanjo, Makalla ameongezea muda ambapo zoezi hilo lililoendeshwa na watumishi wa afya zaidi ya 100, litaendelea hadi kesho Jumatatu.

Makalla amewaomba wananchi kutumia fursa hiyo ili wapate chanjo kwa ajili ya kujikinga na ugonjwa huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!