Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais atoroka na dola mil 169
Kimataifa

Rais atoroka na dola mil 169

Rais wa Afghanistan, Ashraf Ghani
Spread the love

 

RAIS aliyeondolewa madarakani nchini Afghanistan, Ashraf Ghani anadaiwa kubeba dola za Marekani milioni 169. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Rais Ghani ambaye sasa imethibitishwa kuwa ametimkia katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), alitoroka Ikulu ya nchi hiyo iliyopo katika mji mkuu wa Kabul baada ya wanajeshi wa kikundi cha Taliban kuuteka mji huo na miji mingine muhimu.

Kwa mujibu wa Mohammad Zahir Aghbar ambaye ni Balozi wa Afghanistan nchini Tajikstan, Rais Ghani alikuwa amebeba fedha hizo alipotoroka nchi yake siku ya jumapili Agosti 15.

Akizungumza na waandishi wa Habari katika mji mkuu wa Tajik Dushanbe, balozi huyo alisema kuondoka kwa Ghani ni sawa na ‘usaliti kwa taifa lake.’

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!