Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Chakula cha sumu chauwa Watu 24 wa familia moja
Kimataifa

Chakula cha sumu chauwa Watu 24 wa familia moja

Spread the love

 

WATU 24 wa familia moja wamefariki dunia nchini Nigeria, baada ya kula chakula chenye sumu. Inaripoti BBC … (endelea).

Taarifa ya tukio hilo imetolewa jana Jumanne na Kamishna wa Afya wa Jimbo la Sokoto, nchini humo, Ali Inname, akizungumza na waandishi wa habari.

Inname alisema, watu hao walikula chakula chenye sumu ya mbolea aina ya Gishirin Lalle, iliyowekwa katika chakula hicho kimakosa, wakidhani ni chumvi.

Kamishna huyo wa afya, alisema tukio hilo lilitokea Jumatatu, tarehe 9 Agosti 2021.

Hata hivyo, alisema wanafamilia wawili walinusurika kifo kwa kuwa hawakula chakula kingi. Watu hao wanapatiwa matibabu hospitalini.

Inname alishauri wananchi kutenganisha vyakula na vitu vyenye sumu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!