Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe afikishwa Kisutu, ulinzi waimalishwa
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe afikishwa Kisutu, ulinzi waimalishwa

Freeman Mbowe na wenzake wakiwa mahakamani Kisutu
Spread the love

 

KIONGOZI wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu, wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Mbowe na wenzake; Halfani Bwire Hassan, Adam Hassan Kasekwa na Mohammed Abdillahi Lingwenya, wamefikishwa mahakamani hapo mapema leo asubuhi Ijumaa, tarehe 6 Agosti 2021.

Ni baada ya jana Alhamisi, kesi hiyo ilishindwa kuendelea kwa njia ya mtandao ‘video conference’ kusumbua hivyo Hakimu Mwandamizi, Thomas Simba anayesikiliza kesi hiyo, kutoa amri ya washtakiwa hao kufikishwa mahakamani.

Tayari Mbowe na wenzake wamekwisha fikishwa katika chumba cha mahakama.

https://youtu.be/_TllnMb86HI

Kama ilivyokuwa jana Alhamisi, ulinzi umeimalishwa na leo ni zaidi kwani baadhi ya viongozi wa Chadema wanazuiwa kuingia mahakamani.

Askari kazu na waliovalia sare, wameizunguka mahakama hiyo na wengine wamesimama juu ya mahakama hiyo.

Baadhi ya viongozi walioingia ni; Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!