Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Simba wauwa Wanafunzi watatu Arusha
Habari Mchanganyiko

Simba wauwa Wanafunzi watatu Arusha

Spread the love

 

WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Ngoile wilayani Ngorongoro, Mkoa wa Arusha, wameuawa kwa kushambuliwa na Simba, walipokuwa wanatafuta mifugo yao iliyopotea porini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Taarifa ya tukio hilo imetolewa leo Alhamisi, tarehe 5 Agosti 2021 na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo, akizungumza na wanahabari.

Kamanda Masejo amesema, wanafunzi hao ambao ni Olobiko Metui (10), Ndaskoi Sangu (9) na Sanka Saning’o (10), waliuawa tarehe 3 Agosti mwaka huu.

Amesema wanafunzi hao waliokuwa darasa la tatu, walienda porini kuitafuta mifugo hiyo, wakitokea nyumbani kwao baada ya kurudi kutoka shule.

Kamanda Masejo amesema, mwanafunzi mmoja, Kiambwa Lektony (11), alifanikiwa kutoroka katika mashambulizi ya Simba, ambaye anapatiwa matibabu katika Zahanati ya Kata ya Olbalbal, mkoani humo.

“Miili ya marehemu wote imefanyiwa uchunguzi wa kidaktari na imeshakabidhiwa kwa ndugu zao kwa ajili ya mazishi,” amesema Kamanda Masejo.

Kamanda Masejo amewataka wafugaji wasiwape watoto majukumu ya kuchunga mifugo, hasa katika maeneo ya vijiji vinavyopakana na hifadhi za wanayamapori, ili kuokoa maisha yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!