Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yaja na mikakati kupeleka mawasiliano mipakani
Habari Mchanganyiko

Serikali yaja na mikakati kupeleka mawasiliano mipakani

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imeanzisha mikakati ya kumaliza changamoto za mawasiliano, katika maeneo ya pembezoni mwa nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mikakati hiyo imetajwa leo tarehe 26 Julai 2021 na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk. Faustine Ndugulile, akizindua Studio za Redio Jamii inayosimamiwa na Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC), jijini Dodoma.

Waziri huyo wa mawasiliano amesema, mkakati wa kwanza ni kupunguza gharama za leseni za redio zilizopo au zitakazoanzishwa katika maeneo hayo.

“Tunakwenda kupunguza gharama za leseni kwa redio zitakazokuwa ngazi ya wilaya, jamii na katika maeneo ya pembezoni. Tunataka katika maeneo yote yale ambayo wenzetu wamekuwa wanasikiliza redio nchi jirani, tuondokane nayo,” amesema Dk. Ndugulile.

Dk. Faustin Ndungulile

Mkakati mwingine uliotajwa na Dk. Ndugulile, ni kutoa tenda za miradi ya mawasiliano ya simu, katika maeneo hayo.

“Tumetoa tenda ya mawasiliano katika mawasiliano ya simu, maeneo ambayo yako pembezoni mwa nchi. Tayari zabuni tumetangaza ili makampuni ya simu yawekeze katika usikivu wa simu kwenye maeneo hayo,” amesema Dk. Ndugulile.

Dk. Ndugulile amesema, mikakati hiyo imelenga kuwaondolea wananchi wa maeneo ya pembezoni, changamoto ya kupata mawasiliano kutoka katika vyombo vya mawasiliano vya nchi jirani.

“Lengo letu muda mfupi ujao mawasiliano yanayosikika yawe ya Tanzania, badala ya sasa maeneo ya pembezoni kumekuwa na usikivu wa mawasiliano ya nchi jirani,” amesema Dk. Ndugulile.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

error: Content is protected !!