Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yaja na mikakati kupeleka mawasiliano mipakani
Habari Mchanganyiko

Serikali yaja na mikakati kupeleka mawasiliano mipakani

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imeanzisha mikakati ya kumaliza changamoto za mawasiliano, katika maeneo ya pembezoni mwa nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mikakati hiyo imetajwa leo tarehe 26 Julai 2021 na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk. Faustine Ndugulile, akizindua Studio za Redio Jamii inayosimamiwa na Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC), jijini Dodoma.

Waziri huyo wa mawasiliano amesema, mkakati wa kwanza ni kupunguza gharama za leseni za redio zilizopo au zitakazoanzishwa katika maeneo hayo.

“Tunakwenda kupunguza gharama za leseni kwa redio zitakazokuwa ngazi ya wilaya, jamii na katika maeneo ya pembezoni. Tunataka katika maeneo yote yale ambayo wenzetu wamekuwa wanasikiliza redio nchi jirani, tuondokane nayo,” amesema Dk. Ndugulile.

Dk. Faustin Ndungulile

Mkakati mwingine uliotajwa na Dk. Ndugulile, ni kutoa tenda za miradi ya mawasiliano ya simu, katika maeneo hayo.

“Tumetoa tenda ya mawasiliano katika mawasiliano ya simu, maeneo ambayo yako pembezoni mwa nchi. Tayari zabuni tumetangaza ili makampuni ya simu yawekeze katika usikivu wa simu kwenye maeneo hayo,” amesema Dk. Ndugulile.

Dk. Ndugulile amesema, mikakati hiyo imelenga kuwaondolea wananchi wa maeneo ya pembezoni, changamoto ya kupata mawasiliano kutoka katika vyombo vya mawasiliano vya nchi jirani.

“Lengo letu muda mfupi ujao mawasiliano yanayosikika yawe ya Tanzania, badala ya sasa maeneo ya pembezoni kumekuwa na usikivu wa mawasiliano ya nchi jirani,” amesema Dk. Ndugulile.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!