Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia amlilia Mhandisi Mfugale
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia amlilia Mhandisi Mfugale

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Mhandisi Patrick Mfugale. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Mhandisi Mfugale, alifikwa na mauti jana Jumanne, saa 5:00 asubuhi, tarehe 29 Juni 2021, katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma.

Hadi anafikwa na mauti, amehudumu nafasi ya mtendaji mkuu kwa zaidi ya miaka kumi, kuanzia tarehe 23 Mei 2011, akiwa amesimamia ujenzi wa barabara zaidi ya kilomita 1,400 na madaraka mbalimbali yakiwemo ya juu.

Katika ukurasa wake wa Twitter, Rais Samia ameandika “Nimesikitishwa na taarifa ya kifo cha Mhandisi Patrick Mfugale (Mtendaji Mkuu-TANROADS).”

“Nitaukumbuka mchango mkubwa katika ujenzi wa miundombinu yetu hasa barabara, madaraja, reli na umeme.”

“Pole kwa Familia na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi. Mungu amweke mahali pema peponi, Amina.”

Awali, jana Jumanne usiku, taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ilisema, taratibu za mazishi zitatangazwa baadae.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

error: Content is protected !!