Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Makalla amtaka Kamanda Muliro kukomesha uhalifu Dar
Habari Mchanganyiko

Makalla amtaka Kamanda Muliro kukomesha uhalifu Dar

Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Amos Makalla amemuagiza Kamanda mpya wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro kuhakikisha anakomesha uhalifu mkoani humo. Anaripoti Jemima Samwel, DMC … (endelea).

Muliro amehamishiwa mkoani humo hivi karibuni akitoka Mkoa wa Mwanza kwa nafasi hiyo hiyo na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro.

Kamanda Muliro amechukua nafasi ya Kamishna Camilius Wambura ambaye aliteuliwa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI).

Amos Makala

Makalla ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa huo, amekutana na Kamanda Muliro, ofisini kwake leo Jumanne, tarehe 8 Juni 2021.

Makalla amemuelekeza Kamanda Muliro kuendelea na operesheni ya kuwashughulikia kikamilifu majambazi na wahalifu mkoani humo ili Dar es Salaam ibaki kuwa tulivu na wananchi wafanye shughuli zao kwa usalama.

Aidha Makalla amesema, kwa sasa hali ya usalama Dar es Salaam ni shwari na hataki kusikia majambazi yakifanya uhalifu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!