Thursday , 23 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais wa Ufaransa achapwa kofi hadharani
Kimataifa

Rais wa Ufaransa achapwa kofi hadharani

Spread the love

 

RAIS wa Ufaransa, Emmanuel Macron, amejikuta katika wakati mgumu, baada ya kupigwa kofi la uso na mwananchi, katika ziara yake ya kikazi, aliyoifanya nchini humo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Leo Jumanne tarehe 8 Juni 2021, katika mitandao ya kijamii, imesambaa video inayomuonesha Rais Macron akikumbwa na mkasa huo, alipotembelea shule moja ya hoteli iliyoko katika ji wa Tain-I’Hermitage, nje ya Jiji la Valence.

Inadaiwa tukio hilo limetokea mapema leo, wakati Rais Macron akiwasalimia wananchi walio fika kuhudhuria ziara yake, ambapo mwanamume mmoja baada ya kupewa mkono na kiongozi huyo, kama ishara ya salamu, alimnasa kofi la shavuni.

Baada ya mwanaume huyo kumnasa kofi Rais Macron, walinzi wake waliingilia kati na kumtoa kiongozi huyo eneo la tukio.

Kwa mujibu wa mitandao ya kimataifa, watu wawili wamekamatwa kufuatia tukio hilo.

Hata hivyo, haijaelezwa sababu za mwanaume huyo kumpiga Rais Macron.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Raila Odinga: Tutafanya maandamano makubwa mara mbili kwa wiki

Spread the love KIONGOZI wa upinzani nchini Kenya, Raila Amollo Odinga ametangaza...

Kimataifa

Magharibi kuwekeza silaha Indo-Pacific, China yachochea

Spread the love KUVUNJIKA ushirhikiano wa China na Magharibi uliodumu kwa takribani...

Kimataifa

Ruto amlaumu Odinga kujaribu kuanzisha mgogoro kwa mara ya pili

Spread the love  RAIS wa Kenya William Ruto amesema kwamba hatakubali “kutoijali...

Kimataifa

Putin, Xi Jinping kujadili mpango kumaliza vita nchini Ukraine

Spread the love  Vladimir Putin amesema atajadili mpango wenye vipengele 12 wa...

error: Content is protected !!