Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Makalla amtaka Kamanda Muliro kukomesha uhalifu Dar
Habari Mchanganyiko

Makalla amtaka Kamanda Muliro kukomesha uhalifu Dar

Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Amos Makalla amemuagiza Kamanda mpya wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro kuhakikisha anakomesha uhalifu mkoani humo. Anaripoti Jemima Samwel, DMC … (endelea).

Muliro amehamishiwa mkoani humo hivi karibuni akitoka Mkoa wa Mwanza kwa nafasi hiyo hiyo na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro.

Kamanda Muliro amechukua nafasi ya Kamishna Camilius Wambura ambaye aliteuliwa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI).

Amos Makala

Makalla ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa huo, amekutana na Kamanda Muliro, ofisini kwake leo Jumanne, tarehe 8 Juni 2021.

Makalla amemuelekeza Kamanda Muliro kuendelea na operesheni ya kuwashughulikia kikamilifu majambazi na wahalifu mkoani humo ili Dar es Salaam ibaki kuwa tulivu na wananchi wafanye shughuli zao kwa usalama.

Aidha Makalla amesema, kwa sasa hali ya usalama Dar es Salaam ni shwari na hataki kusikia majambazi yakifanya uhalifu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!