Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Migogoro hifadhi za wanyamapori yafukuzisha askari 61
Habari Mchanganyiko

Migogoro hifadhi za wanyamapori yafukuzisha askari 61

Spread the love

 

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dk. Damas Ndumbaro, amesema Askari wa Hifadhi za Wanyamapori 61 wamefukuzwa kazi, huku 40 wakisimamishwa kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili, ikiwemo kukiuka maadili yao ya kazi na kuanzisha migogoro baina ya wananchi na hifadhi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Dk. Ndumbaro ameyasema hayo leo Jumamosi, tarehe 5 Juni 2021, bungeni jijini Dodoma ,akijibu malalamiko ya wabunge kuhusu migogoro hiyo, katika mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022.

“Wizara tumeanza kuchukua hatua, askari 61 tumewafukuza kazi na askari 40 wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi. Moja kati ya kazi ya kwanza mimi kufanya, ni kwenda Ifakara mkoani Morogoro, kufukuza kazi askari watatu,” amesema Dk. Ndumbaro.

Dk. Ndumbaro ametoa wito kwa wananchi wanaofanyiwa vitendo vya ukiukwaji haki za binadamu na askari hao, watoe taarifa kwa ajili ya Serikali kuchukua hatua.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Damas Ndumbaro

“Mkakati wetu ni rahisi kutokomeza vitendo hivyo, tukipata malalamiko yenye ushahidi usio na shaka tunaitisha paredi tunamfukuza. Hatupendi askari aliyepata mafunzo anakiuka miiko ya kazi yake, tunachohitaji ushirikiano kutoka kwa wananchi na wabunge,” amesema Dk. Ndumbaro.

Dk. Ndumbaro amesema, kuanzia Julai Mosi 2021, Askari wa Hifadhi za Wanayamapori watakaobainika kukiuka maadili yao ya kazi na kusababisha migogoro, watapelekwa katika Mahakama za Kijeshi, kwa ajili ya kuchukuliwa hatua.

“Ninasaini kanuni hizo Jumatatu tarehe 7 Juni 2021, ili kuanzia tarehe 1 Julai askari atakayekiuka miiko ya kazi haendi kwenye mahakama za kawaida, anaenda mahakama za kijeshi na anafukuzwa kazi mara moja. Hii naamini italeta ufumbuzi kwenye hoja hii,” amesema Dk. Ndumbaro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!