Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Panga la Ma-RPC laja
Habari Mchanganyiko

Panga la Ma-RPC laja

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema atawaondoa Makamanda wa Jeshi la Polisi wa Mikoa (RPC), watakaoshindwa kudhibiti vitendo vya uhalifu, hasa ujambazi wa kutumia silaha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Jumanne tarehe 18 Mei 2021, akifungua Kiwanda cha Ushonaji cha Polisi, Kurasini mkoani Dar es Salaam.

Kiongozi huyo wa Tanzania amesema udhibiti wa uhalifu huo, utakuwa miongoni mwa vigezo vya kuteua au kutengua uteuzi wa Ma-RPC, atakaoufanya hivi karibuni.

“Jeshi la Polisi mjipange vizuri kukabiliana na hawa wanaotaka kuwajaribu na hii sio hapa  Dar Es Salaam,  bali nchi nzima.

https://www.youtube.com/watch?v=048gTByfeQ0

Na hapa niwe mkweli kwamba, miongoni mwa vigezo nitakavyotumia kuteua au kutengua makamanda wa mikoa ni udhibiti wa vitendo vya ujambazi ikiwemo kutumia silaha,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema “hii nayo itakuwa moja kati ya vigezo, najua IGP (Simon Sirro) umeniletea majina kadhaa kwa ajili ya kamisheni mbili,  ya fedha na lojistiki na ile kamisheni nyingine.  Lakini hiki kitakuwa kimoja kati ya vigezo nitakavyotumia.”

Aidha, Rais Samia amemuagiza Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro, aweke mikakati ya kudhibiti vitendo vya ujambazi.

IGP Simon Sirro

“Changamoto za kiusalama bado zipo nielekeze wanaojaribu kina cha maji kwa kutaka kurejesha vitendo vya ujambazi hapa nchini,  waache. Nampongeza IGP  tarehe 8 Mei alikutana na Maafisa wa Polisi kuweka mikakati kukabiliana nao,” amesema Rais Samia na kuongeza:

“Ni matumaini yangu tutaona matunda ingawa bado tunasikia vijitaarifa taraifa hawa watu wanaendelea kubonyeza, naomba muwe wagumu wanapobonyeza pasibonyee, mliweza kule nyuma hamna sababu ya kushindwa sasa hivi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!