Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kodi ya mishahara yashushwa 1%
Habari za Siasa

Kodi ya mishahara yashushwa 1%

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amepunguza Kodi ya Mshahara (PAYE), kutoka asilimia tisa hadi nane. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Ametangaza punguzo hilo leo Ijumaa, katika maadhimisho ya Mei Mosi ya 2021, iliyofanyika Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.

“Serikali imesikia ombi la kupunguza kodi ya mishahara na tumepunguza asilimia moja kutoka tisa hadi nane. Mtakatwa ninyi pamoja na mimi,” amesema Rais Samia

Pia, ameahidi kulifanyia kazi, suala la malipo yasiyokuwa ya mishahara kukatwa kodi.

https://www.youtube.com/watch?v=vjbNTGs9Kso

“Hakuna nchi iliyosonga mbele kimaendeleo bila kuwategemea wafanyakazi, ndiyo wanajenga miundombinu na kutoa huduma mbalimbali za kijamii. Serikali itaendelea kutatua changamoto zenu mbalimbali,” alisema.

Kuhusu nyongeza ya mishahara, Rais Samia amesema, atapandisha katika maadhimisho kama hayo mwaka 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!