Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kodi ya mishahara yashushwa 1%
Habari za Siasa

Kodi ya mishahara yashushwa 1%

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amepunguza Kodi ya Mshahara (PAYE), kutoka asilimia tisa hadi nane. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Ametangaza punguzo hilo leo Ijumaa, katika maadhimisho ya Mei Mosi ya 2021, iliyofanyika Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.

“Serikali imesikia ombi la kupunguza kodi ya mishahara na tumepunguza asilimia moja kutoka tisa hadi nane. Mtakatwa ninyi pamoja na mimi,” amesema Rais Samia

Pia, ameahidi kulifanyia kazi, suala la malipo yasiyokuwa ya mishahara kukatwa kodi.

https://www.youtube.com/watch?v=vjbNTGs9Kso

“Hakuna nchi iliyosonga mbele kimaendeleo bila kuwategemea wafanyakazi, ndiyo wanajenga miundombinu na kutoa huduma mbalimbali za kijamii. Serikali itaendelea kutatua changamoto zenu mbalimbali,” alisema.

Kuhusu nyongeza ya mishahara, Rais Samia amesema, atapandisha katika maadhimisho kama hayo mwaka 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!