Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kodi ya mishahara yashushwa 1%
Habari za Siasa

Kodi ya mishahara yashushwa 1%

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amepunguza Kodi ya Mshahara (PAYE), kutoka asilimia tisa hadi nane. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Ametangaza punguzo hilo leo Ijumaa, katika maadhimisho ya Mei Mosi ya 2021, iliyofanyika Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.

“Serikali imesikia ombi la kupunguza kodi ya mishahara na tumepunguza asilimia moja kutoka tisa hadi nane. Mtakatwa ninyi pamoja na mimi,” amesema Rais Samia

Pia, ameahidi kulifanyia kazi, suala la malipo yasiyokuwa ya mishahara kukatwa kodi.

https://www.youtube.com/watch?v=vjbNTGs9Kso

“Hakuna nchi iliyosonga mbele kimaendeleo bila kuwategemea wafanyakazi, ndiyo wanajenga miundombinu na kutoa huduma mbalimbali za kijamii. Serikali itaendelea kutatua changamoto zenu mbalimbali,” alisema.

Kuhusu nyongeza ya mishahara, Rais Samia amesema, atapandisha katika maadhimisho kama hayo mwaka 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!