Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Askofu Gwajima aeleza kiini cha nchi kukwama
Habari za Siasa

Askofu Gwajima aeleza kiini cha nchi kukwama

Askofu Josephat Gwajima, Mbunge wa Kawe
Spread the love

 

ASKOFU Josephat Gwaji, Mbunge wa Kawe, Dar es Salaam amesema, Afrika ikiwemo Tanzania haziwezi kuendelea kwa kuwa, hazina utaratibu wa kuendeleza agenda za awamu zilizopita. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Amesema, ili Tanzania ipige hatua, inahitajika mjadala wa kitaifa sambamba na kutafsiri maana ya maendeleo kwa miaka 30 au 50.

Askofu Gwajima ametoa kauli hiyo leo tarehe 15 Aprili 2021, wakati akichangia Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2021/22.

“Ili tuendelee tunahitaji ajenda ya Taifa. Lazima tutafsiri maendeleo ya Tanzania kwa miaka 30 au 50, tuwe na vitu tunaita maendeleo.

“Kama hatujafanya hivi, tuna hatari kwa sababu Katiba yetu inampa nafasi kila rais anayeingia madarakani kwa namna yake, kwa hekima yake na kwa namna ya kutafsiri yeye maendeleo ya Tanzania,” amesema Askofu Gwajima.

Akichangia bungeni hapo, Askofu Gwajima amehoji, nchi inawezaje kusonga mbele wakati hakuna muendelezo wa mikakati na juhudi za waliotangulia?

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!