Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ateua, atumbua bosi TPDC
Habari za Siasa

Rais Samia ateua, atumbua bosi TPDC

Thobias Mwesiga Richard
Spread the love

 

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Thobias Mwesiga Richard. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Richard aliteuliwa jana usiku Jumapili, tarehe 4 Aprili 2021, kushika nafasi hiyo.

Ikiwa ni saa chache zimepita tangu kuteuliuwa, leo Jumatatu asubuhi, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa amesema, Rais Samia ametengua uteuzi huo na kumrejesha Dk. James Mataragio.

Dk. Mataragio, amerejeshwa kuendelea kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TPDC.

Dk. Mataragio ndiye alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa TPDC kabla ya uteuzi Richard kutangazwa jana Jumapili na ametakiwa kuendelea na majukumu yake mara moja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!