Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Bashiru, wenzake waapishwa bungeni
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Bashiru, wenzake waapishwa bungeni

Spread the love

 

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amewaapisha wabunge watatu akiwemo Dk. Bashiru Ally. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Walioapishwa ni; Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, Balozi Libareta Mulamula na Dk. Bashiru.

Wabunge hao wameapishwa leo Alhamisi tarehe 01 Aprili 2021, bungeni jijini Dodoma baada ya jana Jumatano, kuteuliwa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Bashiru alikuwa Katibu Mkuu Kiongozi, nafasi aliyoitumikia kwa siku 32 kuanzia tarehe 27 Februari hadi jana Jumatano.

Mbali na kumteua Balozi Mulamula kuwa mbunge, alimteua kuwa waziri wa mambo ya nje huku Balozi Mbarouk kuwa naibu waziri wa mambo ye nje.

Kabla ya uteuzi huo, Mbarouk alikuwa Balozi wa Tanzania katika Falme za Kiarabu (UAE).

Katika shughuli hiyo ya kuapishwa, Balozi Mulamula alionekana mwenye furaha tangu anaingia na kumaliza kuapishwa akicheza cheza, hali iliyowafanya wabunge kushangilia.

Mara baada ya kumaliza kuapishwa, Spika Ndugai amewapongeza wabunge hao na kuwakaribisha bungeni wabunge hao wapya.

“Mawaziri ninyi ni wabunge, mikiwa huko nje mjue nafasi yenu,” amesema Spika Ndugai

Spika Ndugai amesema, kutokana na mabadiliko yaliyofanywa ya baraza la mawaziri “leo hatukakuwa na maswali na majibu ili kutoa nafasi kwa walioteuliwa kuapishwa na kukabidhiwa ofisi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!