Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mawaziri watatu hawajaguswa tangu 2015 
Habari za Siasa

Mawaziri watatu hawajaguswa tangu 2015 

Wiliam Lukuvi, aliyekuwa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Jamii
Spread the love

 

LICHA Baraza la Mawaziri kufanyiwa mabadiliko mara kadhaa tangu mwaka 2015, mawaziri watatu na naibu waziri mmoja bado hawajaguswa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Mawaziri wasioguswa katika wizara zao tangu utawala wa Rais John Magufuli mwaka 2015, ni Jenista Mhagama ambaye ni Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu,.

Wengine ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi na naibu wake, Angelina Mabula. Pamoja na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako.

Tarehe 31 Machi 2021, Rais Samia Suluhu Hassan alifanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri.

Prof. Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu

Kiongozi huyo mpya wa Tanzania, alitangaza mabadiliko hayo Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, katika hafla ya kumuapisha Dk. Phillip Mpango, aliyemteua kuchukua nafasi yake ya Makamu wa Rais.

Enzi za uongozi wa Dk. Magufuli alifanya mabadiliko  madogo ya baraza la mawaziri zaidi ya mara mbili, ikiwemo 2015, 2019 na 2020, ambapo kuna mawaziri na naibu waziri ambao hawakuguswa, hadi katika mabadiliko yaliyofanywa jana na Rais Samia.

Katika mabadiliko ya baraza hilo, Rais Samia ameongeza naibu waziri mmoja katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ambapo Mwanaidi Ally Hamis amekuwa Naibu Waziri anayeshughulikia Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu wa Bunge), Jenister Mhagama

Awali, katika wizara hiyo alikuwa Dk. Dorothy Gwajima (waziri) na Dk. Godwin Mollel (naibu waziri).

Pia, Wizara ya Uwekezaji aliitoa katika Ofisi ya Rais na kuihamishia katika Ofisi ya Waziri Mkuu.

Rais Samia ameapishwa kuchukua uongozi wan chi kufuatia kifo cha Dk. Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho mkoani Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!