Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kikwete alivyomzungumzia Magufuli, ampongeza Rais Samia
Habari za Siasa

Kikwete alivyomzungumzia Magufuli, ampongeza Rais Samia

Rais John Magufuli akiwa na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete
Spread the love

 

RAIS mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete amesema, kifo cha aliyekiwa Rais wa Taifa hilo, Dk. John Pombe Magufuli, kimewashtua wengi nani pigo kubwa. Anaripoti Matrida Peter, Dar es Salaam … (endelea).

Kikwete aliyekuwa Rais kati ya mwaka 2005 hadi 2015 kisha akamwachia kijiti Dk. Magufuli, imemchukua takribani siku mbili, kuzungumzia kifo hicho.

Dk. Magufuli (61), alifikwa na mauti saa 12 jioni ya Jumatano tarehe 17 Machi 2021, akiwa Hospitali ya Mzena, Makumbusho mkoani Dar es Salaam, akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa mfumo wa umeme wa moyo.

Mwili wake, utazikwa nyumbani kwao Chato mkoani Geita, Alhamisi ijayo tarehe 25 Machi 2021.

Kufuatilia kifo hicho, aliyekuwa makamu wake, Samia Suluhu Hassan, ameapishwa leo Ijumaa tarehe 19 Machi 2021, katika hafla iliyofanyika Ikulu ya Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Kikwete.

Katika ukurasa wake wa Twitter, Kikwete ameandika “Nimepata tabu kuandika kwa kifupi kuelezea simanzi na masikitiko yangu kwa msiba mkubwa ulioukumba nchi yetu kwa kuondokewa na mpendwa wetu Mheshimiwa Rais John Magufuli.”

“Nimelazimika kuyaambatisha hapa chini. Mwenyezi Mungu amuweke mahala pema, peponi,” amesema

Undani wa alichokiandika ikiwa ni pamoja na kutoa nasaha kwa Rais mpya Samia, soma hapa chini;

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!