Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kifo cha Magufuli: Rais Kagame “nimempoteza rafiki”
Kimataifa

Kifo cha Magufuli: Rais Kagame “nimempoteza rafiki”

Spread the love

 

RAIS wa Rwanda, Paul Kagame amesema, mchango uliotolewa na aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli (61) kwa taifa hilo “hauwezi kusahaulika.” Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Kagame ametumia ukurasa wake wa Twitter, kutoa salamu hizo za rambirambi, kufuatia kifo cha Rais Magufuli, aliyefariki dunia jana Jumatano saa 12:00 jioni, katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho, mkoani Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akitangaza msiba huo alisema, Rais Magufuli, alifikwa na mauti wakati akiendelea na matibabu ya mfumo wa umeme wa moyo.

Rais Kagare amesema “nasikitika kumpoteza kaka na rafiki, Rais Magufuli. Mchango wake kwa nchi yetu hauwezi kusahaulika.”

“Tunatuma salamu za rambirambi kwa familia na wananchi wa Tanzania. Wananchi wa Rwanda wako pamoja na Watanzania katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo,” amesema Rais Kagame

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!