Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kifo cha Magufuli: Rais Kagame “nimempoteza rafiki”
Kimataifa

Kifo cha Magufuli: Rais Kagame “nimempoteza rafiki”

Spread the love

 

RAIS wa Rwanda, Paul Kagame amesema, mchango uliotolewa na aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli (61) kwa taifa hilo “hauwezi kusahaulika.” Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Kagame ametumia ukurasa wake wa Twitter, kutoa salamu hizo za rambirambi, kufuatia kifo cha Rais Magufuli, aliyefariki dunia jana Jumatano saa 12:00 jioni, katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho, mkoani Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akitangaza msiba huo alisema, Rais Magufuli, alifikwa na mauti wakati akiendelea na matibabu ya mfumo wa umeme wa moyo.

Rais Kagare amesema “nasikitika kumpoteza kaka na rafiki, Rais Magufuli. Mchango wake kwa nchi yetu hauwezi kusahaulika.”

“Tunatuma salamu za rambirambi kwa familia na wananchi wa Tanzania. Wananchi wa Rwanda wako pamoja na Watanzania katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo,” amesema Rais Kagame

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!