Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Michezo Mshambuliaji Dodoma jiji ashinda tuzo
Michezo

Mshambuliaji Dodoma jiji ashinda tuzo

Spread the love

 

ANWARI Jabir, mshambuliaji wa Dodoma Jiji, ameshinda tuzo ya mchezaji bora mwezi Februari 2021, kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mshambuliaji huyo, amechukua tuzo hiyo mara baada ya kuwashinda mshambuliaji wa KMC, Charles Ilanfya na Issa Ngoah wa Dodoma Jiji.

Ndani ya mwezi Februari, Anwari aliisaidia timu yake ya Dodoma Jiji kushinda michezo mitano na kutoka sare mmoja huku akiweka kambani mabao manne.

Kwa sasa Dodoma Jiji iko nafasi ya tano ya msimamo ikiwa na pointi 32.

Anwari anakuwa mchezaji wa tano kutwaa tuzo hiyo toka mwezi Septemba 2020, wakati Ligi hiyo inaanza.

Wachezaji wengine ambao tayari wameshatwaa tuzo hiyo ni Price Dube (Septemba-Azam), Mukoko Tonombe (Oktoba- Yanga), John Bocco (Novemba- Simba), Saido Ntibanzokiza (Desemba- Yanga) na Deogratius Mafie (Januari-Biashara United).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Michezo

Piga pesa na mechi za UEFA

Spread the love  HATIMAYE leo hii ndio kitaeleweka nani aende Nusu Fainali...

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

error: Content is protected !!