Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Mshambuliaji Dodoma jiji ashinda tuzo
Michezo

Mshambuliaji Dodoma jiji ashinda tuzo

Spread the love

 

ANWARI Jabir, mshambuliaji wa Dodoma Jiji, ameshinda tuzo ya mchezaji bora mwezi Februari 2021, kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mshambuliaji huyo, amechukua tuzo hiyo mara baada ya kuwashinda mshambuliaji wa KMC, Charles Ilanfya na Issa Ngoah wa Dodoma Jiji.

Ndani ya mwezi Februari, Anwari aliisaidia timu yake ya Dodoma Jiji kushinda michezo mitano na kutoka sare mmoja huku akiweka kambani mabao manne.

Kwa sasa Dodoma Jiji iko nafasi ya tano ya msimamo ikiwa na pointi 32.

Anwari anakuwa mchezaji wa tano kutwaa tuzo hiyo toka mwezi Septemba 2020, wakati Ligi hiyo inaanza.

Wachezaji wengine ambao tayari wameshatwaa tuzo hiyo ni Price Dube (Septemba-Azam), Mukoko Tonombe (Oktoba- Yanga), John Bocco (Novemba- Simba), Saido Ntibanzokiza (Desemba- Yanga) na Deogratius Mafie (Januari-Biashara United).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!