Wednesday , 1 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Gharama kipimo cha corona Z’bar yapaa
Afya

Gharama kipimo cha corona Z’bar yapaa

Spread the love

 

KUPIMA virusi vya corona (COVID-19), visiwani Zanzibar sasa ni Dola za Marekani 80 (zaidi ya Sh.180,00), badala ya Sh.30,000 za awali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Katika taarifa iliyotolewa na wizara ya afya visiwani humo jana Jumapili tarehe 28 Februari 2021, imeeleza bei hiyo mpya itakuwa kwa watu wote bila kutenganisha raia kutoka mataifa ya nje na wale wa ndani ya nchi.

Gharama za awali za kipimo hicho Zanzibar kwa wageni kutoka bje ya Afrika ilikuwa Dola za Marekani 80, wageni kutoka Afrika Mashariki 45,000 na raia wa visiwa hivyo Sh. 30,000.

Taarifa ya wizara hiyo inaeleza, msafiri yeyote atatakiwa kupima siku tatu kabla ya kusafiri kama ambavyo utaratibu wa awali ulivyokuwa.

Wizara hiyo imeelekeza hospitali zitakazotoa huduma hiyo ni pamoja na Migombani, Lumumba, Hospitali ya Blobal, Unguja. Pemba ina kituo kimoja ambacho ni Mfikiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

error: Content is protected !!