Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Pikipiki 16 zakamtwa Dar, 10 mbaroni
Habari

Pikipiki 16 zakamtwa Dar, 10 mbaroni

Spread the love

WATU 10 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, kwa tuhuma za kujihusisha na wizi wa pikipiki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza na wanahabari leo Jumatatu tarehe 1 Machi 2021 jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa amesema, watuhumiwa hao wamekamatwa katika operesheni maalumu ya kusaka wezi wa pikipiki.

“Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kuanzia tarehe 1 hadi 28 Februari 2021, lilifanya oparesheni maalum ya kuwasaka wezi wa pikipiki na kufanikiwa kuwakamata wakiwa na pikipiki 16 zidhaniwazo kuwa za wizi,” amesema Kamanda Mambosasa.

Miongoni mwa watuhumiwa hao ni, Stephen Paul (38), Mkazi wa Ulongoni A, Salum Mustafa (28), Mkazi wa Kigogo na Nsajigwa Kaisi (25), Mkazi wa Mongo la Ndege A.

“Oparesheni hiyo ilifanyika baada ya kupokea taarifa toka kwa wahanga wa matukio hayo ambayo yalikithiri katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.

“Aidha watuhumiwa hao wamekuwa wakiiba pikipiki katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam na kuzipeleka kwa madalali ili kuziuza sehemu mbalimbali,” amesema Kamanda Mambosasa.

Kamanda Mambosasa amesema, Jeshi la Polisi, Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na oparesheni ya msako wa wizi wa pikipiki, magari na wahalifu wa makosa mengine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

Habari

Tanzania yaungana na nchi 180 kushiriki maonesho ya utalii Ujerumani

Spread the love  TANZANIA imeungana na mataifa 180 duniani kushiriki maonesho makubwa...

error: Content is protected !!