DAKTARI Bashiru Ally, Katibu Mkuu Kiongozi amesema, taarifa za kuteuliwa kwake, kwa mara ya kwanza alizipata kupitia mitandaoni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Ametoa kauli hiyo leo tarehe 27 Februari 2021, wakati akiapishwa kushika wadhifa huo Ikulu, jijini Dar es Salaam.
“Jana jioni niko nasoma mafaili yangu, napata taarifa kupitia kwenye mitandao kwamba umeniteua.
“Mshtuko huo hauniwezeshi niseme, bado natafakari sana nitafanya nini, nifanye nini kukidhi maratajio yako kwa imani uliyonipa mfululizo,” Dk. Bashiru alimueleza Rais John Magufuli.
Pia amemshukuru Rais Magufuli kwa kumwamini huku akimuahidi, kuwa hatomuangusha katika nafasi hiyo aliyomteua.
“Nakushukuru kwa imani yako kubwa, hii ni mara ya pili kwa kunipa wadhifa mkubwa; kwanza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na sasa utendaji ndani ya serikali, imani hiyo nitailipa kwa imani,” amesema Dk. Bashiru.
Dk. Bashiru aliteuliwa jana kushika wadhifa huo uliokuwa umeshikiliwa na Balozi John Kijazi, aliyefariki dunia tarehe 17 Februari 2021. Kabla ya uteuzi huo, Dk. Bashiru alikuwa Katibu Mkuu wa CCM.
Leave a comment