Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mauaji ya Jamal Khashoggi, CIA yaivua nguo Saudia Arabia
Kimataifa

Mauaji ya Jamal Khashoggi, CIA yaivua nguo Saudia Arabia

Mwandishi Jamal Khashoggi enzi za uhai wake
Spread the love

 

RIPOTI mpya iliyotolewa na shirika la kijasusi la Marekani (CIA), imemtaja mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudia Arabia, Mohammed Bin Salman, ndiye mhusika mkuu wa mauaji ya mwandishi habari, Jamal Khashoggi (59). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Khashoggi alifariki duni mwaka 2018, katika ubalozi wa Saudia, mjini Intanbul, nchini Uturuki,

Ripoti hiyo ya shirika la kijasusi iliyotolewa na utawala wa Rais Joe Biden, imeeleza kuwa Bin Salman aliidhinisha operesheni ya kumkamata; na au kumuua Khashoggi, mjini Istanbul, nchini Uturuki.

Waziri wa Mambo ya nchi za nje wa Marekani, Antony Blinken amesema, kufuatia kupatikana kwa taarifa hiyo, serikali ya mjini Washington, itachukua mwelekeo mpya wa kisera kwa taifa hilo la Saudia.

Hata hivyo, serikali mjini Riyadh na mwanamfalme mwenyewe, wamekana kuhusika na mauaji hayo na kusema, taarifa hiyo imejaa uzushi na inatathmini isiyokubalika kuhusu utawala wa falme.

Serikali ya Saudia imekuwa ikieleza kuwa mauaji ya Khashoggi kwenye ubalozi wake mdogo, nchini Uturuki, yalifanywa katika operesheni ya kihalifu na inakanusha mwanamfalme Salman kuhusika na mauaji hayo.

Aidha, Saudi Arabia inapinga kile inachokiita, “kuingiliwa kwa utawala wake na uhuru wa mfumo wake wa mahakama.”

“Ripoti hii, imekuwa na hitimisho lisilo sahihi. Imetolewa wakati falme hii imekwisha kosoa uhalifu huo wa kutisha, na uongozi wa Saudia umechukua hatua zinazohitajika kuhakikisha kisa kama hicho hakitokei tena,” imeeleza taarifa ya wizara ya mambo ya kigeni ya taifa hilo.

Mrithi huyo wa kiti cha ufalme –  Mohammed Bin Salman – ameendelea  kukanusha madai hayo, pamoja na washauri wake kadhaa wa karibu, kutiwa hatiani kwa mauaji hayo na mamlaka za sheria nchini humo.

Jamal Khashoggi aliyekuwa uhamishoni Marekani akiandika ripoti zinazomkosoa Mohammed Salman na serikali ya Saudia, aliuwawa tarehe 2 Oktoba 2018.

Mwandishi huyo alielezwa na balozi wa Saudia afike katika ubalozi wa taifa hilo mjini Istanbul, ili aweze kupatiwa nyaraka kadhaa alizokuwa akizihitaji kumuwezesha kufunga ndoa na mpenzi wake Hatice Cengiz, raia wa Uturuki.

Wakati Saudia ikikana kuhusika na mauaji hayo, ripoti ya kijasusi imesheheni ushahidi unaonyesha ushirka wa Bin Salman katika mauaji hayo.

Saudi Arabia, ni mshirika muhimu wa Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati.

CIA inaeleza kwa kujiamini, kwamba Bin Salman, ndiye aliyeamuru mauaji hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!