Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dorothy ‘akabidhiwa’ kiti cha Maalim Seif
Habari za Siasa

Dorothy ‘akabidhiwa’ kiti cha Maalim Seif

Dorothy Semu, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT wazalendo Bara
Spread the love

 

KAMAMU Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Bara, Dorothy Semu amekaimu rasmi kiti cha uenyekiti wa chama hicho, kilichokuwa kikishikiliwa na Hayati Maalim Seif Sharif Hamad, aliyefariki dunia hivi karibuni. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Maalim Seif, aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho Taifa, alifariki dunia tarehe 17 Februari 2021 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), jijini Dar es Salaam ambapo mwili wake ulizikwa tarehe 18 Februari 2021 kijijini kwao Nyali-Mtambwe, Kisiwani Pemba.

Taarifa ya Semu kukaimu nafasi ya Hayati Maalim Seif, imetolewa Jumatatu tarehe 22 Februari 2021 na Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma ACT-Wazalendo, Salim Bimani.

Taarifa ya Bimani imesema, hatua hiyo ni matakwa ya Ibara ya 84 (3) na (4) ya  Katiba ya ACT-Wazalendo ya 2015,  Toleo la 2020.

Maalim Seif Sharrif Hamad, aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo

“Ibara hiyo inasomeka kama ifuatavyo, 84 (3); iwapo mwenyekiti wa chama hayupo kwa sababu yoyote ile basi makamu mwenyekiti ambaye anatoka upande mwingine wa muungano tofauti ns anaotoka mwenyekiti, na kama makamu mwenyekiti aliyetajwa kwanza naye hayupo, basi makamu mwenyekiti aliyebakia atakaimu nafasi ya uenyekiti,” imesema taarifa ya Bimani.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bimani, Semu atakaimu nafasi hiyo katika kipindi kisichozidi miezi 12, hadi pale Mwenyekiti mpya atakapochaguliwa na Mkutano Mkuu Maalumu wa Taifa.

“Kwa kuzingatia Ibara ya 84 (4) ya Katiba ya ACT-Wazalendo, Dorothy Semu ataendelea kukaimu nafasi hiyo kwa kipindi kisichozidi miezi 12 hadi pale mwenyekiti moya atakapochaguliwa na Mkutano Maalumu wa Taifa,” imesema taarifa ya Bimani.

Hayati Maalim Seif alichaguliwa na ACT-Wazalendo kuwa mwenyekiti wa chama hicho tarehe 14 Machi 2020, nafasi aliyoitumika hadi umauti ulipomkuta.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!