Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dorothy ‘akabidhiwa’ kiti cha Maalim Seif
Habari za Siasa

Dorothy ‘akabidhiwa’ kiti cha Maalim Seif

Dorothy Semu, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT wazalendo Bara
Spread the love

 

KAMAMU Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Bara, Dorothy Semu amekaimu rasmi kiti cha uenyekiti wa chama hicho, kilichokuwa kikishikiliwa na Hayati Maalim Seif Sharif Hamad, aliyefariki dunia hivi karibuni. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Maalim Seif, aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho Taifa, alifariki dunia tarehe 17 Februari 2021 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), jijini Dar es Salaam ambapo mwili wake ulizikwa tarehe 18 Februari 2021 kijijini kwao Nyali-Mtambwe, Kisiwani Pemba.

Taarifa ya Semu kukaimu nafasi ya Hayati Maalim Seif, imetolewa Jumatatu tarehe 22 Februari 2021 na Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma ACT-Wazalendo, Salim Bimani.

Taarifa ya Bimani imesema, hatua hiyo ni matakwa ya Ibara ya 84 (3) na (4) ya  Katiba ya ACT-Wazalendo ya 2015,  Toleo la 2020.

Maalim Seif Sharrif Hamad, aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo

“Ibara hiyo inasomeka kama ifuatavyo, 84 (3); iwapo mwenyekiti wa chama hayupo kwa sababu yoyote ile basi makamu mwenyekiti ambaye anatoka upande mwingine wa muungano tofauti ns anaotoka mwenyekiti, na kama makamu mwenyekiti aliyetajwa kwanza naye hayupo, basi makamu mwenyekiti aliyebakia atakaimu nafasi ya uenyekiti,” imesema taarifa ya Bimani.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bimani, Semu atakaimu nafasi hiyo katika kipindi kisichozidi miezi 12, hadi pale Mwenyekiti mpya atakapochaguliwa na Mkutano Mkuu Maalumu wa Taifa.

“Kwa kuzingatia Ibara ya 84 (4) ya Katiba ya ACT-Wazalendo, Dorothy Semu ataendelea kukaimu nafasi hiyo kwa kipindi kisichozidi miezi 12 hadi pale mwenyekiti moya atakapochaguliwa na Mkutano Maalumu wa Taifa,” imesema taarifa ya Bimani.

Hayati Maalim Seif alichaguliwa na ACT-Wazalendo kuwa mwenyekiti wa chama hicho tarehe 14 Machi 2020, nafasi aliyoitumika hadi umauti ulipomkuta.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!