Tuesday , 30 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya COVID-19: Ureno yaelemewa, yaomba msaada Ujeruman  
Afya

COVID-19: Ureno yaelemewa, yaomba msaada Ujeruman  

Spread the love

KASI ya kuenea kwa virusi vya corona (COVID-19) nchini Ureno, inatikisa taifa hilo. Inaripoti mitandao ya kimataifa… (endelea).

Serikali ya Ureno baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya, iliamuwa kuomba msaada kutoka Serikali ya Ujerumani.

Wizara ya Ulinzi ya Ujerumani imeafiki kutuma maofisa wa afya wa jeshi lake, pamoja na vifaa vya matibabu nchini Ureno ili kukabiliana na hali hiyo.

Taarifa kutoka Ureno zinaeleza, vyumba vya wagonjwa mahututi vimeelemewa baada ya kuongezeka kwa maambukizi ya virusi hivyo.

Gazeti la Ujerumani la Der Speigel, limeripoti kuwa jeshi hilo linapanga kupeleka madaktari na maofisa wa matibabu 27 Ureno, na kwamba maofisa hao watakuwepo Ureno kwa siku tatu.

Pia vitu vitakavyopelekwa Ureno kutoka Ujerumani ni pamoja na vitanda pia mashine za kusaidia kupumua.

Serikali ya Ureno imeeleza, vimebakia vitanda saba pekee ambavyo havina wagonjwa mahututi kati ya 850.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

error: Content is protected !!