Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Ni mbwembwe, ‘wabunge wa Chadema’ wakitinga bungeni
Habari za Siasa

Ni mbwembwe, ‘wabunge wa Chadema’ wakitinga bungeni

Baadhi ya wabunge waliofukuzwa Chadema wakiingia bungeni
Spread the love

 

WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wamewakaribisha wabunge kutoka Chama cha ACT-Wazalendo na wale waliotimuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kwa nderemo. Anaripoti Ragina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Ni baada ya Job Ndugai, Spika wa Bunge kutoa taarifa ya kuwakaribisha ambapo wale wa ACT-Wazalendo walitangulia na kufuatiwa 19 waliofukuzwa Chadema kwa madai ya usaliti.

Hii ni baada ya wale wa CCM walioteuliwa na Rais John Magufuli kutanguliwa. Wabunge hao ni Humphrey Polepole, Riziki Lulida, Dk. Dorothy Gwajima na Prof. Shukrani Manya.

Wakati wabunge hao 19 na wanne wa ACT-Wazalendo wakiingia ukumbini kwa makundi, walipigiwa meza na idadi kubwa ya wabunge wa CCM kuashiria kuwakaribisha.

Wabunge hao 19 wanaotajwa na Bunge kuwa ni wa Chadema ni Halima Mdee, Ester Bulaya, Esther Matiko, Nusrat Hanje, Grace Tendega.

Wengine ni Hawa Mwaifunga, Jesca Kishoa, Agnesta Lambat. Tunza Malapo. Ceciia Pareso, Asia Mwadin Mohamed, Felister Njau, Naghenjwa Kaboyoka, Sophia Mwakagenda, Kunti Majala, Stella Siyao, Salome Makamba, Anatropia Theonest na Conchesta Lwamlaza.

Wabunge wa ACT-Wazalendo ni Khatibu Saidi Haji (Konde), Salum Mohamed Shafi (Chonga), Omar Ali Omar (Wete) na Khalifa Mohamed Issa (Mtambwe).

Mdee na Bulaya wameingia bungeni wakiwa na mavazi meusi huku wakivaa barakoa kwa ajili ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19).

Pia wabunge hao wawili (Mdee na Bulaya), hawakuingia na wenzao hapo awali, walichelewa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!