Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Michezo Kocha mpya Simba: Namjua Kagere
Michezo

Kocha mpya Simba: Namjua Kagere

Spread the love

 

KOCHA mpya wa timu ya Simba, Didier Gomes amesema kuwa ameifuatilia kwa karibu Ligi Kuu ya Tanzania Bara na kuwafahamu baadhi ya wachezaji ikiwemo Meddie Kagere ambaye alimfundisha alipokuwa kwenye klabu ya Rayol Sport ya nchini Rwanda. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kocha huyo ametua nchini jana na kujiunga na klabu ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili leo Jumapili 24 Januari 2021.

Wakati akijibu swali la mwandishi wa habari kwa namna gani ameifuatilia Ligi Kuu ya Tanzania na kujibu kuwa ameifuatilia Ligi hii kwa muda mrefu kwa kuwa inaendelea kukua taratibu kwa siku za hivi karibuni.

“Naijua na nimeifuatilia Ligi ya Tanzania kwa kuwa ni moja ya Ligi nzuri na inakuwa kila siku na hata hivyo nawajua baadhi ya wachezaji akiwemo Meddie Kagere ambaye nilimfundisha nikiwa nchini Rwanda nikiwa na klabu ya Rayon Sports,” alisema kocha huyo.

Kagere ambaye alikuwa hapati nafasi ya kuanza kwenye kikosi cha kwanza cha kocha aliyeondoka kutokana na mfumo wake wa kutumia mshambuliaji mmoja na kuamua kumtumia zaidi John Bocco.

Pengine ujio wa Gomes huenda ukampa tena nafasi mchezaji huyo ambaye alikuwa mfungaji bora wa klabu hiyo pamoja na Ligi Kuu kwenye msimu uliomalizika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!