Monday , 29 May 2023
Home Kitengo Michezo Kocha mpya Simba: Namjua Kagere
Michezo

Kocha mpya Simba: Namjua Kagere

Spread the love

 

KOCHA mpya wa timu ya Simba, Didier Gomes amesema kuwa ameifuatilia kwa karibu Ligi Kuu ya Tanzania Bara na kuwafahamu baadhi ya wachezaji ikiwemo Meddie Kagere ambaye alimfundisha alipokuwa kwenye klabu ya Rayol Sport ya nchini Rwanda. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kocha huyo ametua nchini jana na kujiunga na klabu ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili leo Jumapili 24 Januari 2021.

Wakati akijibu swali la mwandishi wa habari kwa namna gani ameifuatilia Ligi Kuu ya Tanzania na kujibu kuwa ameifuatilia Ligi hii kwa muda mrefu kwa kuwa inaendelea kukua taratibu kwa siku za hivi karibuni.

“Naijua na nimeifuatilia Ligi ya Tanzania kwa kuwa ni moja ya Ligi nzuri na inakuwa kila siku na hata hivyo nawajua baadhi ya wachezaji akiwemo Meddie Kagere ambaye nilimfundisha nikiwa nchini Rwanda nikiwa na klabu ya Rayon Sports,” alisema kocha huyo.

Kagere ambaye alikuwa hapati nafasi ya kuanza kwenye kikosi cha kwanza cha kocha aliyeondoka kutokana na mfumo wake wa kutumia mshambuliaji mmoja na kuamua kumtumia zaidi John Bocco.

Pengine ujio wa Gomes huenda ukampa tena nafasi mchezaji huyo ambaye alikuwa mfungaji bora wa klabu hiyo pamoja na Ligi Kuu kwenye msimu uliomalizika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

NBC Dodoma Marathon yazinduliwa, wakiambiaji 6,000 kushiriki

Spread the loveBENKI ya NBC imetangaza kufanyika kwa mbio kubwa za NBC...

Michezo

Rais Samia anunua tiketi 5000 Yanga vs USM Alger

Spread the loveRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu...

Michezo

Mwenyekiti UVCCM anogesha nusu fainali Kimwanga CUP, Hawa Abdul Rede CUP kwa kishindo

Spread the loveHEKAHEKA za michuano ya kuwania kuingia fainali ya michuano ya...

Michezo

Yanga SC. yatwaa ubingwa wa pili mfululizo

Spread the love  KLABU ya Yanga SC imeweka rekodi ya kutwaa ubingwa...

error: Content is protected !!