Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Jerry Murro: Alisema atajiua
Habari Mchanganyiko

Jerry Murro: Alisema atajiua

Spread the love

 

JERRY Murro, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha amesema, kijana Furahini Mbise, aliyekutwa amekufa katika Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Maweni, jijini humo aliwahi kusema “nitajiua.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Amesema, ameagiza Jeshi la Polisi pamoja na Daktari Kiongozi wa wilaya hiyo, kufanya uchunguzi ili kubaini nini kilitokea mpaka kijana huyo kupoteza maisha.

“Asili ya kijana huyu aliyekufa, hata ukiuliza kijijini, watakwambia kuina baadhi ya nyakati alisema anataka kujiua,” amesema Murro.

Akizungumzia mkasa ulivyokuwa, mkuu huyo wa wilaya amesema, Furahini alifariki dunia akiwa amehifadhiwa kwenye chumba kimoja kilichopo kwenye ofisi ya mtendaji huo kabla ya kujinyonga.

 “Taarifa zilizopo, kijana yule aliitwa saa 12 asubuhi kwa mwenyekiti wa kitongoji kuzungumza changamoto yao wenyewe ya mgogoro wa shami la kukatia majani.

“…na walipofika pale, kijana huyu ambaye amefariki, alileta vurugu. Alienda akachukua panga, mwenyekiti akaogopa akasema hili jambo liende kwa mtendaji,” amesema Murro.

Ameeleza, waliambiwa waende kwenye ofisi ya mtendaji kwa ajili ya kuzungumza jambo hilo.

“Taarifa zinaeleza, kijana yule alipofika ofisi ya mtendaji alileta vurugu, ndio wakaamua wamuweke kwenye chumba cha pembeni cha stoo, na alipowekwa kwenye chumba hicho habari zinasema, aliamua kujitundika, kujiua, kujinyonga,” amesema.

Kiongozi huyo amesema, awali alizungumza na ndugu wa marehemu akiwemo dada yake, pacha wa marehemu kama kulikuwa na mgogoro kati yake (marehemu) na mtendaji wa kata.

“Nikawauliza kama kulikuwa na mgogoro kati ya mtendaji wetu na marehemu, wakasema hapakuwa na mgogoro. Sasa iweje leo watu waseme amekwenda kwenye ofisi ya mtendaji, mtendaji akamuua? anaanzaje kumuua? mtu ambaye hakuwa na mgogoro naye?

“Lakini taarifa ambazo hazina mashaka, kijana huyu alikuwa na asili ya vurugu, ndio maana hata kwa mwenyekiti wa kitongoji jambo lake lilishindikana kusikilizwa, ndio likaletwa kwa mtendaji wa kata,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!