Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi ajinyoga ndani mwake
Habari Mchanganyiko

Polisi ajinyoga ndani mwake

Kitanzi
Spread the love

ASKARI wa Kituo cha Polisi Kibaha mkoani Pwani, Yusuph Mohamed Said (52), amekutwa amejinyonga nyumbani kwake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Pwani … (endelea). 

Taarifa ya tukio hilo, imetolewa jana Jumanne tarehe 19 Januari 2021, na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa, wakati anazungumza na wanahabari mkoani humo.

Akielezea tukio hilo, Kamanda Nyigesa amesema, limetokea jioni ya tarehe 18 Januari 2021.

“Askari wa cheo cha Koplo namba E6472, Yusuph Mohamed Said, ana miaka 52, alikuwa anafanya shughuli za uaskari katika Kituo cha Polisi Kibaha.”

“Tarehe 18 Januari 2021 majira ya saa 12 jioni, amekutwa katika nyumba yake inayoendelea na ujenzi, akiwa amejinyonga,” alisema Kamanda Nyigesa.

Kamanda Nyigesa alisema, uchunguzi wa tukio hilo unaendelea kufanywa na Jeshi la Polisi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa (katikati)

Alisema Jeshi la Polisi mkoani humo linafanya maandalizi ya kuusafirisha mwili wake kwenda kwao mkoani Lindi, kwa ajili ya mazishi.

“Jeshi la Polisi tunaendelea na uchunguzi wa kifo hiki cha marehemu.  Tunafanya maandalizi ya kumsafirisha kwao mkoani Lindi kwa mazishi,” alisema Kamanda Nyigesa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

error: Content is protected !!