Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Mwinyi ateua Ma DC
Habari za Siasa

Rais Mwinyi ateua Ma DC

Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Hussein Mwinyi, amefanya uteuzi wa wakuu wa wilaya (DC) kumi visiwani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Uteuzi huo ameufanya jana Jumatatu tarehe 28 Desemba 2020 na kutangazwa kwa umma na Hassan Khatib Hassan, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu ya Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa ya Hassan, uteuzi wa wakuu hao wa wilaya, ulianza jana Jumatatu.

Walioteuliwa na wilaya zao kwenye mabano ni, Rajab Ali Rajab (Mjini). Kabla ya uteuzi huo, Rajab alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B.

Khamis Mbeto Khamis (Magharibi A), Hamida Mussa Khamis (Magharibi B), Aboud Hassan Mwinyi (Kaskazini A), Kassim Haidar Jabir (Kaskazini B), Sadifa Juma Khamisi (Kusini-Unguja) na Marina Joel Thomas (Kati). Kabla ya uteuzi huo, Marina alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mjini.

Wengine ni; Mgeni Khatib Yahya (Wete), Mohammes Mussa Seif (Micheweni). Kabla ya uteuzi huo, Seif alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Wete na Abdallah Rashid Ali  ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Chakechake).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!