Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Mwinyi ateua Ma DC
Habari za Siasa

Rais Mwinyi ateua Ma DC

Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Hussein Mwinyi, amefanya uteuzi wa wakuu wa wilaya (DC) kumi visiwani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Uteuzi huo ameufanya jana Jumatatu tarehe 28 Desemba 2020 na kutangazwa kwa umma na Hassan Khatib Hassan, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu ya Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa ya Hassan, uteuzi wa wakuu hao wa wilaya, ulianza jana Jumatatu.

Walioteuliwa na wilaya zao kwenye mabano ni, Rajab Ali Rajab (Mjini). Kabla ya uteuzi huo, Rajab alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B.

Khamis Mbeto Khamis (Magharibi A), Hamida Mussa Khamis (Magharibi B), Aboud Hassan Mwinyi (Kaskazini A), Kassim Haidar Jabir (Kaskazini B), Sadifa Juma Khamisi (Kusini-Unguja) na Marina Joel Thomas (Kati). Kabla ya uteuzi huo, Marina alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mjini.

Wengine ni; Mgeni Khatib Yahya (Wete), Mohammes Mussa Seif (Micheweni). Kabla ya uteuzi huo, Seif alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Wete na Abdallah Rashid Ali  ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Chakechake).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!