Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yataka majibu ya corona kwa saa 24
Habari Mchanganyiko

Serikali yataka majibu ya corona kwa saa 24

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imeagiza utoaji wa majibu ya vipimo vya ugonjwa wa corona ndani ya saa 24 badala ya saa 72. Anaandika Regina Mkonde…(endelea).

Akizungumza na Uongozi wa Maabara ya Taifa na Afya ya Jamii, Prof. Abel Makubi ambaye ni Mganga Mkuu wa Serikali leo tare he 26 Desemba 2020 amesema, hatua hiyo itaondoa malalamiko ya ucheleweshwaji kwa wale wanaotaka kusafiri.

Prof. Makubi amekutana na uongozi wa maabara hiyo, wasimamizi wa maabara na waganga wakuu kutoka hospitali za serikali na binafsi.

Ni baada ya kufanya ziara katika maabara hiyo kwa lengo la kusikiliza na kuangalia namna ya kutatua changamoto zinazokabili maabara hiyo.

“Ucheleweshaji wa majibu kamwe hauwezi kuvumiliwa,” amesema Prof. Makubi huku akisisitiza kuwepo malalamiko hayo hasa kutoka kwa wasafiri.

Ameutaka uongozi wa maabara hiyo kufanya lolote linalowezekana kuhakikisha wanatimiza la kutoa majibu ya vipimo vya corona ndani ya saa 24.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

error: Content is protected !!