Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yataka majibu ya corona kwa saa 24
Habari Mchanganyiko

Serikali yataka majibu ya corona kwa saa 24

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imeagiza utoaji wa majibu ya vipimo vya ugonjwa wa corona ndani ya saa 24 badala ya saa 72. Anaandika Regina Mkonde…(endelea).

Akizungumza na Uongozi wa Maabara ya Taifa na Afya ya Jamii, Prof. Abel Makubi ambaye ni Mganga Mkuu wa Serikali leo tare he 26 Desemba 2020 amesema, hatua hiyo itaondoa malalamiko ya ucheleweshwaji kwa wale wanaotaka kusafiri.

Prof. Makubi amekutana na uongozi wa maabara hiyo, wasimamizi wa maabara na waganga wakuu kutoka hospitali za serikali na binafsi.

Ni baada ya kufanya ziara katika maabara hiyo kwa lengo la kusikiliza na kuangalia namna ya kutatua changamoto zinazokabili maabara hiyo.

“Ucheleweshaji wa majibu kamwe hauwezi kuvumiliwa,” amesema Prof. Makubi huku akisisitiza kuwepo malalamiko hayo hasa kutoka kwa wasafiri.

Ameutaka uongozi wa maabara hiyo kufanya lolote linalowezekana kuhakikisha wanatimiza la kutoa majibu ya vipimo vya corona ndani ya saa 24.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!