Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Serikali yataka majibu ya corona kwa saa 24
Habari Mchanganyiko

Serikali yataka majibu ya corona kwa saa 24

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imeagiza utoaji wa majibu ya vipimo vya ugonjwa wa corona ndani ya saa 24 badala ya saa 72. Anaandika Regina Mkonde…(endelea).

Akizungumza na Uongozi wa Maabara ya Taifa na Afya ya Jamii, Prof. Abel Makubi ambaye ni Mganga Mkuu wa Serikali leo tare he 26 Desemba 2020 amesema, hatua hiyo itaondoa malalamiko ya ucheleweshwaji kwa wale wanaotaka kusafiri.

Prof. Makubi amekutana na uongozi wa maabara hiyo, wasimamizi wa maabara na waganga wakuu kutoka hospitali za serikali na binafsi.

Ni baada ya kufanya ziara katika maabara hiyo kwa lengo la kusikiliza na kuangalia namna ya kutatua changamoto zinazokabili maabara hiyo.

“Ucheleweshaji wa majibu kamwe hauwezi kuvumiliwa,” amesema Prof. Makubi huku akisisitiza kuwepo malalamiko hayo hasa kutoka kwa wasafiri.

Ameutaka uongozi wa maabara hiyo kufanya lolote linalowezekana kuhakikisha wanatimiza la kutoa majibu ya vipimo vya corona ndani ya saa 24.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Ditopile aungana na Wana-Kongwa kwa Iftar, wamuombea dua Rais Samia

Spread the loveKATIKA muendelezo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Mbunge wa Viti...

Habari Mchanganyiko

PSSSF yawekeza kwenye viwanda 4, kuzalisha ajira 3,000

Spread the loveKATIKA kuisaidia Serikali kupunguza tatizo la uhaba wa ajira nchini,...

Habari Mchanganyiko

Luhemeja ahimiza utunzaji rasilimali maji kwa faida ya vizazi vijavyo

Spread the love  NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Cyprian Luhemeja...

Habari Mchanganyiko

NSSF yawapa darasa wahariri uwekezaji wa nyumba, yapewa cheti

Spread the loveMFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umetoa wito...

error: Content is protected !!