Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yaibwaga CCM, ACT-Wazalendo
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yaibwaga CCM, ACT-Wazalendo

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeshinda Tuzo ya Watu, Taasisi na Chapa, zinazoongoza mtandaoni (Tanzania Digital Awards), kwenye kipengele cha chama bora cha siasa  mtandaoni (Best Political Party Use of Social Media). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Chadema kimetwaa tuzo hiyo baada ya kupata kira nyingi katika kipengele hicho cha  chama bora cha siasa, katika kutumia teknolojia ya kidigitali kuchochea maendeleo.

Chama hicho kimevibwaga vyama vitatu vilivyokua vinachuana katika  kundi F, kwenye kipengele cha uongozi bora katika teknolojia ya kidigitali.

Tuzo hiyo ilitangazwa jana tarehe 25 Desemba 2020.

 

Vyama vilivyokuwa vinasaka tuzo hiyo ni, ACT-Wazalendo, Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF).

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa

Tuzo hiyo imetolewa kwa mara ya kwanza nchini Tanzania mwaka huu.

Katika tuzo hiyo, wananchi walipiga kura kuchagua chama cha siasa bora katika kutumia mitandao ya kijamii kuongoza wananchi kwenye kuleta maendeleo.

Tuzo hizo zinalenga kutambua mchango wa watu na taasisi ambazo zinatumia kifanisi na kwa ubunifu majukwaa na teknolojia za kidigitali kuhamasisha na kuchagiza maendeleo ya kudumu katika mitandao na jamii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!