Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto atoka hospitalini ‘narudi kwenye kampeni’
Habari za Siasa

Zitto atoka hospitalini ‘narudi kwenye kampeni’

Spread the love

KIONGOZI wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe ameruhusiwa kutoka Hospitali ya Aga Khani jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa kwa matibabu baada ya kupata ajali ya gari. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Zitto na watu wengine wanne walipata ajali ya gari akitoka Kata ya Kalya kwenda Lukoma kwenye mkutano wa kampeni Jimbo la Kigoma Kusini 6 Oktoba 2020.

Baada ya kutokea kwa ajali hiyo, majeruhi wote walipatiwa huduma ya kwanza Kituo cha Afya cha Kalya kabla ya kuhamishiwa Hospitali ya Maweni mkoani Kigoma na baadaye Hospitali ya Aga Khan.

Leo Jumamosi tarehe 10 Oktoba 2020, Zitto ameandika katika ukura wake wa Twitter ameandika “nimeruhusiwa kutoka hospitali. Nawashukuru madaktari na wauguzi Kituo cha Afya Kalya – Uvinza, Hospitali ya Maweni Kigoma na Hospitali ya Aga Khan Dar es Salaam.”

Zitto ambaye ni mgombea ubunge wa Kigoma Mjini amesema “asanteni sana wote kwa Dua, Sala na maombi yenu. Nataraji kurudi kwenye kampeni siku chache zijazo In Sha Allah.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!