Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Samatta njia panda Aston Villa
Michezo

Samatta njia panda Aston Villa

Mbwana Samatta
Spread the love

NAHODHA wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ Mbwana Samatta anayekipiga kwenye klabu ya Astorn Villa huenda akauzwa katika dirisha hili kubwa la usajili kufuatia uongozi wa klabu hiyo kumsajili Ollie Watkins kutoka klabu ya Brentford. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Samatta mwenye umri wa miaka 27, alijiunga na Astorn Villa kwenye dirisha dogo la usajili mwezi Januari akitokea klabu ya Genk inayoshiriki Ligi Kuu nchini Ubelgiji.

Baadhi ya vyombo vya habari kutoka nchini Uingereza vimeripoti kuwa Samatta ni moja ya wachezaji watakaondoka kwenye klabu kabla ya dirisha la usajili kufungwa 4 Oktoba, 2020 licha ya kudumu kwa miezi nane.

Taarifa zinaeleza kuwa huenda mshambuliaji huyo akatimkia kwenye klabu ya Besiktas inayoshiriki Ligi Kuu nchini Uturuki ambayo imeonesha nia ya kuhitaji huduma ya mshambuliaji huyo.

Maamuzi ya kuondoka baadhi ya nyota ndani ya klabu hiyo yamekuja baada ya kocha mkuu wa timu hiyo, Dean Smith kutaka kufanya marekebisho kwenye kikosi hicho kabla ya dirisha la usajili kufungwa.

Mpaka sasa mshambuliaji huyo amecheza jumla ya michezo 14 toka ajiunge na Astorn villa kwenye Ligi Kuu na kufunga bao moja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!