SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imezitaka klabu zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara kuwasilisha wasifu na vyeti vya makocha wao waliowaajili kuvinoa vikosi vyao. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa kutoka ndani ya shirikisho hilo imeeleza kuwa wasifu na vyeti vya vinavyohitajika ni vya kocha mkuu, kocha msaidizi, kocha wa viungo na kocha wa makipa.
Ikumbukwe taarifa hiyo inakuja huku baadhi ya timu zikiwa zimefanya usajili wa wachezaji na makocha kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi 2020/21 ulioanza 6 septemba, 2020.
Aidha shirikisho hilo limesema kuwa nakala hizo zinahitajika kuwasilishwa kwa ofisi ya mkurugenzi wa ufundi ndani ya Tff, huku mwisho wa zoezi hilo ikiwa 15 Septemba, 2020.
Leave a comment