Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema, TBC wamaliza tofauti zao
Habari za Siasa

Chadema, TBC wamaliza tofauti zao

Spread the love

MGOGORO baina ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), umemalizika baada ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) kuwakutanisha viongozi wakuu wa taasisi hizo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Kikao cha viongozi hao kimefanyika leo Ijumaa tarehe 4 Septemba 2020 jijini Dar es Salam chini ya Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Dk. Wilson Mahera.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema, Dk. Ayubu Ryioba, Mkurugenzi Mkuu wa TBC na Kaimu Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile.

Kila upande umeelezea kilichotokea na kwa pamoja kukubaliana kusameheana na kusonga mbele.

Msingi wa kikao hicho unatokana na Mbowe wakati wa uzinduzi wa kampeni za urais za Chadema zilizofanyika tarehe 28 Agosti 2020 Viwanja vya Zakhiem Mbagala Dar es Salaam, alitoa dakika 15 kwa waandishi wa TBC kuondoka mkutanoni hapo.

Mbowe alitoa agizo hilo akiwatuhumu kukatisha matangazo mara kwa mara wakati wakirusha moja kwa moja ‘live’ uzinduzi huo akisema, hali hiyo inawanyika fursa Watanzania kufuatilia mkutano huo.

Taarifa yote ya kilichotokea kwenye kikao hicho iliyotolewa na Katibu TEF, Neville Meena hii hapa;

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!