Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema, TBC wamaliza tofauti zao
Habari za Siasa

Chadema, TBC wamaliza tofauti zao

Spread the love

MGOGORO baina ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), umemalizika baada ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) kuwakutanisha viongozi wakuu wa taasisi hizo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Kikao cha viongozi hao kimefanyika leo Ijumaa tarehe 4 Septemba 2020 jijini Dar es Salam chini ya Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Dk. Wilson Mahera.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema, Dk. Ayubu Ryioba, Mkurugenzi Mkuu wa TBC na Kaimu Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile.

Kila upande umeelezea kilichotokea na kwa pamoja kukubaliana kusameheana na kusonga mbele.

Msingi wa kikao hicho unatokana na Mbowe wakati wa uzinduzi wa kampeni za urais za Chadema zilizofanyika tarehe 28 Agosti 2020 Viwanja vya Zakhiem Mbagala Dar es Salaam, alitoa dakika 15 kwa waandishi wa TBC kuondoka mkutanoni hapo.

Mbowe alitoa agizo hilo akiwatuhumu kukatisha matangazo mara kwa mara wakati wakirusha moja kwa moja ‘live’ uzinduzi huo akisema, hali hiyo inawanyika fursa Watanzania kufuatilia mkutano huo.

Taarifa yote ya kilichotokea kwenye kikao hicho iliyotolewa na Katibu TEF, Neville Meena hii hapa;

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!