Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif: CCM ijiandae kuondoka itake isitake
Habari za Siasa

Maalim Seif: CCM ijiandae kuondoka itake isitake

Maalim Seif Sharrif Hamad, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo amesema, chama hicho kimejiandaa kushika dola na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kijiandae kuondoka ‘taka isitake’ baada ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Faki Sosi, Lindi … (endelea)

Maalim Seif ametoa kauli hiyo leo Jumanne tarehe 1 Septemba 2020 katika mkutano wa uzinduzi wa kampini za urais katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mpilipili.

Bernard Kamilius Membe ndiye mgombea urais na Profesa Omar Fakih Hamad, mgombea mwenza.

Akizindua kampeni hizo, Maalim Seif  amesema, msimamo wa chama hicho sasa ni kukataa kuonewa.

Amesema wagombea wa ACT-Wazalendo wa Tanzania Bara na Zanzibar.

Bernard Membe-ACT-Wazalendo

“Chama cha ACT-Wazalendo sasa kimekuwa ni tishio kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM),  ndio maana wagombea wetu wameenguliwa, msimamo wetu sasa maonevu basi,” amesema Maalim Seif ambaye ni mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama hicho.

“Sasa huu ni wakati wa kuikomboa nchi yetu na mkombozi ni ACT-Wazalendo, tunahitaji serikali itakayoleta maendeleo kwa wananchi, itakayoleta uhuru kwa wananchi na Serikali hiyo itaongozwa na Bernard Kamilius Membe,” amesema Maalim Seif huku akishangiliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!