ZITTO Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo amewataka Watanzania wasikipigie kura Chama Chama Mapinduzi (CCM) kwani kimeshindwa kutekeza ahadi walizoahidi kwenye Kampeni za Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 25 Oktoba 2015. Anaaripoti Faki Sosi, Lindi … (endelea)
Zitto amesema, CCM imekuwa akiahidi lakini haitekelezi na uchaguzi mwingine unapofika inaahidi tena jambo ambalo amewaomba Watanzania siku ya uchaguzi mkuu tarehe 28 Oktoba 2020 kuiweka kando.
Kiongozi huyo wa chama, amesema hayo katika uzinduzi wa kampeni za urais wa chama hicho leo Jumanne tarehe 1 Septemba 2020 katika Viwanja vya Mpilipili Mjini Lindi.
ACT-Wazalendo, imemsimamisha Bernard Membe kuwania urais na Profesa Omar Fakih Hamad, mgombea mwenza.
“CCM iliahidi mikoa ya kusini itakuwa na uchumi wa gesi lakini mpaka sasa haijulikani hili limeishia wapi, Je, watu wa Lindi mmeuona uchumi wa gesi, watu ambao hawakutekeleza ahadi yao mtawachagua tena,” amehoji Zitto na kujibiwa ‘hapana, haiwezekani.
Zitto amesema, CCM ilitoa ahadi ya kutoa Sh. 50 milioni kila kijiji “lakini hakuna kijiji hata kimoja kilichopata fedha na hawa hawa CCM waliahido kutoa ajira milioni moja lakini hawakutekeleza, hivi karibuni wameahidi kutoa kajira milioni sita nazo itakuwa vile vile.”
Amesema kutokana na hilo, chama hicho kimeandaa Ilani itakayonadiwa na mgombea wake wa urais, Membe na mgombea mwenza, Profesa Hamad ambayo ni mkombozi wa wananchi wote.
Zitto ambaye ni mgombea ubunge Kigoma Mjini amesema, katika kipindi cha siku 62 za kampeni, watazunguka nchi nzima kuinadi ilani hiyo kwa Watanzania ili waweze kuwachahua na kuongoza dola.
Leave a comment