Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif: CCM ijiandae kuondoka itake isitake
Habari za Siasa

Maalim Seif: CCM ijiandae kuondoka itake isitake

Maalim Seif Sharrif Hamad, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo amesema, chama hicho kimejiandaa kushika dola na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kijiandae kuondoka ‘taka isitake’ baada ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Faki Sosi, Lindi … (endelea)

Maalim Seif ametoa kauli hiyo leo Jumanne tarehe 1 Septemba 2020 katika mkutano wa uzinduzi wa kampini za urais katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mpilipili.

Bernard Kamilius Membe ndiye mgombea urais na Profesa Omar Fakih Hamad, mgombea mwenza.

Akizindua kampeni hizo, Maalim Seif  amesema, msimamo wa chama hicho sasa ni kukataa kuonewa.

Amesema wagombea wa ACT-Wazalendo wa Tanzania Bara na Zanzibar.

Bernard Membe-ACT-Wazalendo

“Chama cha ACT-Wazalendo sasa kimekuwa ni tishio kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM),  ndio maana wagombea wetu wameenguliwa, msimamo wetu sasa maonevu basi,” amesema Maalim Seif ambaye ni mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama hicho.

“Sasa huu ni wakati wa kuikomboa nchi yetu na mkombozi ni ACT-Wazalendo, tunahitaji serikali itakayoleta maendeleo kwa wananchi, itakayoleta uhuru kwa wananchi na Serikali hiyo itaongozwa na Bernard Kamilius Membe,” amesema Maalim Seif huku akishangiliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!