Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu aibua shangwe mkutano mkuu ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Lissu aibua shangwe mkutano mkuu ACT-Wazalendo

Spread the love

TUNDU Antipus Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ameibua shangwe ndani ya Mkutano Mkuu wa ACT-Wazalendo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mkutano huo unafanyika leo Jumatano tarehe 5 Agosti 2020 katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.

Lissu ameingia ukumbini wakati Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo akijiandaa kutoa hotuba kwa wajumbe wa mkutano huo.

Kabla hajaanza, Lissu ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema-Bara, akaingia ukumbini akiwa ameambatana na mgombea wake mwenza, Salum Mwalimu ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu-Zanzibar.

Shangwe ziliibuka kwa wajumbe kusimama kushangilia wakiimba wimbo maalum wa ACT-Wazalendo huku Lissu akisalimiana na wajumbe na viongozi mbalimbali.

Kabla hajakaa katika nafasi iliyokuwa imeandaliwa, Zitto alimwita Lissu na Bernard Membe, Mshauri Mkuu wa ACT-Wazalendo wapande jukwaani hali iliyoibua shangwe zaidi. Membe anatarajiwa kuteuliwa na mkutano huo kuwa mgombea urais

Watatu hao walikaa jukwaani kwa muda huko wakiimba wimbo na kuwasalimia wajumbe wa mkutano huo.

Katika hotuba yake, Zitto amesema, “nimefurahi kuwaona wagombea wetu wawili wa urais wakiwa pamoja na kwetu sisi kushirikiana ni muhimu na bila kushirikiana itakuwa ni ngumu kuindoa CCM madarakani na itakuwa rahisi mmo kuiondoa CCM madarakani.”

Ziito amesema, “tutaendelea kufanya mazungumzo hadi hatua ya mwisho kuhakikisha tunashirikiana na kuwa na mgombea mmoja.”

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa na habari mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!